Kwa mujibu wa Shirika la Habari la ABNA, kituo cha «i24 News» cha utawala wa Kizayuni kiliripoti: «Nikwamba, matamshi ya Trump na pia kutangazwa kwa mkataba wa maelewano na Iran haikutarajiwa.»
Vyombo hivyo vya habari vya Kizayuni pia vilikiri kwamba hadi sasa hakuna dalili zozote kwamba Iran imetoa makubaliano ya kweli katika mazungumzo.
Pia, waziri wa zamani wa Israel, «Chaim Ramon», amesema: «Makubaliano kati ya Washington na Tehran ni mabaya na yataidhuru Israel, na pia yana athari kwa hatima ya kisiasa ya Netanyahu.»
Mtafiti wa Israel, «Eyal Zisser», katika maandishi yake yenye kejeli kwa Netanyahu aliandika: «Je, sisi ni mamluki tu ambao hutumwa kushambulia malengo na kuvumilia mashambulizi ya makombora inapobidi, kisha tunapohitajika tunatupwa kando?»
Your Comment